web analytics
أخبار عاجلة
Mwenyezi Mungu kuwa Pamoja na Mja Wake, Sababu na Athari zake

Mwenyezi Mungu kuwa Pamoja na Mja Wake, Sababu na Athari zake

Mwenyezi Mungu kuwa Pamoja na Mja Wake, Sababu na Athari zake

خطبة الجمعة لوزراة الأوقاف مسموعة باللغة السواحيلية : الدخول في معية الله عز وجل أسبابه وآثاره ، خطبة الجمعة القادمة ، 3 يناير 2020 م ، 8 جماد الأول 1441 هـ .

 

video


 

Sifa zote njema ni zake Mwenyezi Mungu Mtukufu Mola Mlezi wa Viumbe vyote, anaesema katika Kitabu chake Kitukufu:

 {هُوَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ اسْتَوَى عَلَى الْعَرْشِ يَعْلَمُ مَا يَلِجُ فِي الْأَرْضِ وَمَا يَخْرُجُ مِنْهَا وَمَا يَنْزِلُ مِنَ السَّمَاءِ وَمَا يَعْرُجُ فِيهَا وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنْتُمْ وَاللَّهُ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ }

Yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita; kisha akakaa vyema juu ya enzi. Anayajua yanayo ingia katika ardhi na yanayo toka humo, na yanayo teremka kutoka mbinguni, na yanayo panda humo. Naye yu pamoja nanyi popote mlipo. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona mnayo yatenda.

 

Na ninashuhudia ya kwamba hakuna Mungu mwingine anaestahiki kuabudiwa kwa Haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu yeye pekee asiye na mshirika wake, na ninashuhudia ya kwamba Bwana wetu na Mtume wetu Muhammad ni Mja na Mjumbe wake. Ewe Mola wetu tunakuomba umswalie umrehemu na umbariki yeye na Jamaa zake na Maswahaba wake wote.

 

Na baada ya Utangulizi huu:

 

Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwa karibu na waja wake kunaweza kukawa ni kwa kuwachunga, au kuwasaidia. Kuwachunga kuna maana ya yeye Mtukufu kuvijua vilivyo, Viumbe vyake vyote, ambapo anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَعِندَهُ مَفَاتِحُ الْغَيْبِ لَا يَعْلَمُهَا إِلَّا هُوَ وَيَعْلَمُ مَا فِي الْبَرِّ وَالْبَحْرِ وَمَا تَسْقُطُ مِن وَرَقَةٍ إِلَّا يَعْلَمُهَا وَلَا حَبَّةٍ فِي ظُلُمَاتِ الْأَرْضِ وَلَا رَطْبٍ وَلَا يَابِسٍ إِلَّا فِي كِتَابٍ مُّبِينٍ}

Na ziko kwake funguo za ghaibu; hakuna azijuaye ila Yeye tu. Na Yeye anajua kilioko nchi kavu na baharini. Na halidondoki jani ila analijua. Wala punje katika giza la ardhi, wala kinyevu, wala kikavu ila kimo katika Kitabu kinacho bainisha.

 

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَى ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ وَلَا خَمْسَةٍ إِلَّا هُوَ سَادِسُهُمْ وَلَا أَدْنَى مِن ذَلِكَ وَلَا أَكْثَرَ إِلَّا هُوَ مَعَهُمْ أَيْنَ مَا كَانُوا ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُوا يَوْمَ الْقِيَامَةِ  إِنَّ اللَّهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ}

Kwani huoni kwamba Mwenyezi Mungu anajua vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi? Hauwi mnong’ono wa watu watatu ila Yeye huwa ni wane wao, wala wa watano ila Yeye huwa ni wa sita wao. Wala wa wachache kuliko hao, wala walio wengi zaidi, ila Yeye yu pamoja nao popote pale walipo. Kisha Siku ya Kiyama atawaambia waliyo yatenda. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

 

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{أَلَا يَعْلَمُ مَنْ خَلَقَ وَهُوَ اللَّطِيفُ الْخَبِيرُ }

Asijue aliye umba, naye ndiye Mjua siri, Mwenye khabari.

 

Na ya pili ni: Uwepo wa pamoja wa Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mja wake katika kumsaidia, kukuwafikisha, kumlinda, kumuunga mkono na kumlea. Na amewatengea haya Mitume wake A.S, na Mawalii wake, na Watu wema katika waja wake walio pamoja naye.

     Na hakika Qurani Tukufu imeashiria katika sehemu nyingi Ukaribu huu wa Mja na Mola wake ambao huwa wanaupata Watu Maalumu katika waja wake Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na katika hili, maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Mitume wake wawili, Mtume Musa A.S, na Haruna A.S, ambapo anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 {اذْهَبْ أَنْتَ وَأَخُوكَ بِآيَاتِي وَلَا تَنِيَا فِي ذِكْرِي * اذْهَبَا إِلَى فِرْعَوْنَ إِنَّهُ طَغَى * فَقُولَا لَهُ قَوْلًا لَيِّنًا لَعَلَّهُ يَتَذَكَّرُ أَوْ يَخْشَى * قَالَا رَبَّنَا إِنَّنَا نَخَافُ أَنْ يَفْرُطَ عَلَيْنَا أَوْ أَنْ يَطْغَى * قَالَ لَا تَخَافَا إِنَّنِي مَعَكُمَا أَسْمَعُ وَأَرَى}

Nenda, wewe na ndugu yako, pamoja na ishara zangu, wala msichoke kunikumbuka. Nendeni kwa Firauni. Hakika yeye amepindukia mipaka. Mwambieni maneno laini, huenda akazingatia au akaogopa. Wakasema: Ewe Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tunaogopa asije akapindukia mipaka juu yetu au kufanya jeuri. Akasema: Msiogope! Hakika Mimi ni pamoja nanyi. Nasikia na ninaona.

 

Na Upamoja huu aliouzungumzia Mtume Musa A.S, pale Watu wake walipodhani kuwa Firauni na Wanajeshi wake wamekwishawazingira, na hakuna kimbilio lolote litakalowaokoa na mabavu yake, mbele yao kuna bahari, na Firauni na Wanajeshi wake wako nyuma yao. Hapo wakapiga kelele wakisema:

 

 {إِنَّا لَمُدْرَكُونَ }

Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!

 

Akajibu Musa A.S, huku akiwa na yakini na Imani ya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu na kwamba atamsaidia na atamnusuru. Akasema:

{قَالَ كَلَّا إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهْدِينِ}

(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa

 

Na Uwepo wa Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mja Wake S.A.W, wakati wa Hijirah yake ambapo anasema Bwana wetu Abubakari Siddiiq R.A: Nilikuwa na Mtume S.A.W, Pangoni, nikaiangalia miguu ya Washirikina na Nikasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, kama mmoja wao angeliangalia miguu angetuona, akasema Mtume S.A.W: Ewe Abubakari: Unapofikiria uwili wetu tambua kwamba watatu wetu ni Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na katika hili, anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{إِلَّا تَنْصُرُوهُ فَقَدْ نَصَرَهُ اللَّهُ إِذْ أَخْرَجَهُ الَّذِينَ كَفَرُوا ثَانِيَ اثْنَيْنِ إِذْ هُمَا فِي الْغَارِ إِذْ يَقُولُ لِصَاحِبِهِ لَا تَحْزَنْ إِنَّ اللَّهَ مَعَنَا فَأَنْزَلَ اللَّهُ سَكِينَتَهُ عَلَيْهِ وَأَيَّدَهُ بِجُنُودٍ لَمْ تَرَوْهَا وَجَعَلَ كَلِمَةَ الَّذِينَ كَفَرُوا السُّفْلَى وَكَلِمَةُ اللَّهِ هِيَ الْعُلْيَا وَاللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ}

Ikiwa nyinyi hamtamnusuru Mtume, basi Mwenyezi Mungu alikwisha mnusuru walipo mtoa walio kufuru, naye ni wa pili katika wawili walipo kuwa katika pango, naye akamwambia sahibu yake: Usihuzunike. Hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja nasi. Mwenyezi Mungu akamteremshia utulivu wake, na akamuunga mkono kwa majeshi msiyo yaona, na akalifanya neno la walio kufuru kuwa chini, na Neno la Mwenyezi Mungu kuwa ndilo juu. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye nguvu Mwenye hikima.

 

Utukutu ulioje anapokuwa Mja pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu, na yoyote atakaekuwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu basi hakuna kioicho dhidi yake, kwa yoyote aliye dhidi yake na yule aliye pamoja naye. Na ili Uwepo wa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu upatikane kwa Mja, anapaswa Mja huyu kuingia katika Milango ya kuelekea katika uwepo huo, na lazima atumie njia itakayopelekea kumwezesha Jambo hili, na miongoni mwa Milango hiyo Muhimu ni: Ni kuifikia Imani kamili ya kumwamini Mwenyezi Mungu Mtukufu

Ambapo anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 {وَأَنَّ اللَّهَ مَعَ الْمُؤْمِنِينَ}

Kwani hakika Mwenyezi yu pamoja na Waumini

 

Na hali ya Imani ni kama alivyoitaja Mtume S.A.W: Ni kumwamini Mwenyezi Mungu Mtukufu, na Malaika wake na Vitabu vyake na Mitume wake na Siku ya Mwisho, na Kuamini Qadar, Kheri na Shari yake. Na ukweli wa Imani ni kudhihirika athari zake katika Maadili na Mwenendo wa Mtu na jinsi anavyoishi na Watu, ambapo anasema Mtume S.A.W: Mwislamu ni yule ambaye Watu watasalimika na Ulimi wake na Mikono yake, na Muumini ni yule ambaye Watu watamwamini kwa Maisha na Mali zao.

Na miongoni mwake ni: Ni pale Mja anapofanikisha Uchamungu na Wema wake kwa Watu wote, ambapo anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{إنَّ اللَّهَ مَعَ الَّذِينَ اتَّقَوا وَّالَّذِينَ هُم مُّحْسِنُونَ}

Hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja na wenye kumcha, na watendao mema.

 

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ}

Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu yu pamoja na wachamngu.

 

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَإِنَّ اللَّهَ لَمَعَ الْمُحْسِنِينَ}

Na hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja na watu wema.

 

Ni kitendo cha kila Mja ambacho kinamridhisha Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kujiepusha na kila kinachomuudhi Mwenyezi Mungu Mtukufu. Ni mkusanyiko wa kila jambo la heri. Na Qurani Tukufu imebainisha katia sehemu nyingi, miongoni mwazo ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu aliposema:

{لَيْسَ الْبِرَّ أَن تُوَلُّوا وُجُوهَكُمْ قِبَلَ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَلَكِنَّ الْبِرَّ مَنْ آمَنَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَالْمَلَائِكَةِ وَالْكِتَابِ وَالنَّبِيِّينَ وَآتَى الْمَالَ عَلَى حُبِّهِ ذَوِي الْقُرْبَى وَالْيَتَامَى وَالْمَسَاكِينَ وَابْنَ السَّبِيلِ وَالسَّائِلِينَ وَفِي الرِّقَابِ وَأَقَامَ الصَّلَاةَ وَآتَى الزَّكَاةَ وَالْمُوفُونَ بِعَهْدِهِمْ إِذَا عَاهَدُوا وَالصَّابِرِينَ فِي الْبَأْسَاءِ وَالضَّرَّاءِ وَحِينَ الْبَأْسِ أُولَئِكَ الَّذِينَ صَدَقُوا وَأُولَئِكَ هُمُ الْمُتَّقُونَ}

Sio wema kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi. Bali wema ni wa anaye muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii, na anawapa mali, kwa kupenda kwake, jamaa na mayatima na masikini na wasafiri, na waombao, na katika ugombozi, na akawa anashika Sala, na akatoa Zaka, na wanao timiza ahadi yao wanapo ahidi, na wanao vumilia katika shida na dhara na wakati wa vita; hao ndio walio sadikisha, na hao ndio wajilindao.

 

 Anasema Mtume wetu S.A.W: Msihasidiane, msipandishiane bei katika bidhaa zenu, msibughudhiane, msifanyiane vitimbi, na aziuze yoyote katika nyinyi dhidi ya mauzo ya nduguye, na kuweni Waja wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, ndugu, Mwislamu ndugu yake Mwislamu, hamdhulumu, wala hamtupi na wala hamchukii. Uchamungu uko hapa (kifuani).

 

Na anaashiria kifuani kwake mara tatu, inamtosha mja kupata shari yake anapomchukia ndugu yake Mwislamu. Kila Mwislamu kwa ndugu yake Mwislamu ni haramu. Damu yake, Mali yake na Heshima yake.

Na Nguzo ya Ihsani, Mtume S.A.W, ameibainisha vizuri katika Maneno yake yeye mwenyewe aliposema: Ni Kumwamini Mwenyezi Mungu Mtukufu kama unamwona, na kama Wewe humuoni basi hakika yeye anakuona.

Na hapo, Mja huifikia kikamilifu hali ya kumchunga Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Yakini kamili kwamba Mola wake Mlezi hamsahau yeye katika hali yake ya Siri na ya Wazi, na katika shughuli zake zote na utulivu wake pia.

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 {أَلَمْ يَعْلَم بِأَنَّ اللَّهَ يَرَى} .

Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

 

Na miongoni mwa njia za kuingia katika Kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni: Uvumilivu. Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَاصْبِرُوا إِنَّ اللَّهَ مَعَ الصَّابِرِينَ}

Na subirini. Hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja na wanao subiri.

 

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَبَشِّرِ الصَّابِرِينَ * الَّذِينَ إِذَا أَصَابَتْهُمْ مُصِيبَةٌ قَالُوا إِنَّا لِلَّهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ * أُولَئِكَ عَلَيْهِمْ صَلَوَاتٌ مِنْ رَبِّهِمْ وَرَحْمَةٌ وَأُولَئِكَ هُمُ الْمُهْتَدُونَ}

Na wabashirie wanao subiri, Wale ambao ukiwasibu msiba husema: Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea. Hao juu yao zitakuwa baraka zitokazo kwa Mola wao Mlezi na rehema. Nao ndio wenye kuongoka.

 

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعْيُنِنَا وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ}

Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama.

 

Anasema Mtume S.A.W: Na utambue kwamba kukivumilia unachokichukia kuna heri nyingi sana. Na Uvumilivu ni: kuizuia nafsi yako na huzuni, na kuuzuia ulimi usilalamike na kuvizuia viungo na hasira, na hali hii hupatikana kwa kupambana vikali na nafsi, na kufanya hivyo ni kutoa kitu bora zaidi. Anasema Mtume S.A.W: … Na mwenye kujitahidi kuvumilia basi Mwenyezi Mungu Mtukufu humjaalia uvumilivu, na hajapewa mtu kitu bora  na kipana zaidi kuliko uvumilivu.

Na miongoni mwa njia za kukufikisha katika Kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni: Mzinduko wa dhamira yako; kwani Mtu mwenye Dhamira iliyo hai anatambua fika ya Kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu yuko pamoja naye anapokuwa safarini, au anapokuwa pale anapoishi, au anapokuwa peke yake au na watu, na hakuna kinachofichika kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na wala hakuna siri yoyote au jambo la wazi linalompita.

 

Na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Mtume Yusufu A.S, pale yule Mwanamke alipoifunga Milango ya nyumba, na akamwandalia mazingira ya kufanyia maasi, na Yusufu A.S, akajikinga kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Kipindi chote na ulimi wake ukaanza kukariri na kuisema kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{إِنَّهُ رَبِّي أَحْسَنَ مَثْوَايَ إِنَّهُ لاَ يُفْلِحُ الظَّالِمُونَ}

Huyu bwana wangu kaniweka maskani nzuri, na hakika wenye kudhulumu hawatengenekewi.

 Na hilo ndilo lililotajwa na Mwanamke wa Kiongozi wa Misri kama inavyobainisha Qurani Tukufu kupitia Kauli ya Mwanamke huyo katika Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَلَقَدْ رَاوَدْتُهُ عَنْ نَفْسِهِ فَاسْتَعْصَمْ}

Na kweli mimi nilimtaka naye akakataa.

  Kuhisi kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni jambo Tukufu mno, na lo ni pale Mja anapokuwa na hofu ya Mola wake Mtukufu Duniani, na akaokoka na adhabu yake Mwenyezi Mungu Mtukufu Siku ya Kiama. Na katika Hadithi Qudsiy, anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Kwa Utukufu wangu mimi sikusanyi kwa mja wangu hofu mbili, na wala simkusanyii usalama wa aina mbili; anaponiamini Duniani, nitamwogopesha Siku ya Kiama, na anapo niogopa Duniani basi mimi nitampatia usalama siku ya Kiama.

Mwanadamu pia anabahatika kuingia katika kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kumtaja na kumkumbuka Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{فَاذْكُرُونِي أَذْكُرْكُمْ وَاشْكُرُوا لِي وَلَا تَكْفُرُونِ}

Basi nikumbukeni nitakukumbukeni, na nishukuruni wala msinikufuru.

 Na anasema Mtume wetu S.A.W: Kwamba anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Hadithi Qudsiy: Mimi niko katika dhana ya Mja wangu kwangu mimi, na Mimi niko nae anaponikumbuka, na iwapo atanitaja Mimi katika nafsi yake nami nitamtaja katika Nafsi yangu. Na akinitaja kwa watu, basi nami nitamtaja katika Watu walio bora zaidi…

Ninaisema kauli yangu hii na ninamwomba Mwenyezi Mungu Mtukufu anisamehe mimi na akusameheni nyinyi.

***

Sifa zote njema ni zake Mwenyezi Mungu Mtukufu Mola Mlezi wa viumbe vyote, na ninashuhudia ya kwamba hakuna Mungu mwingine anaestahiki kuabudiwa kwa Haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu yeye pekee asiye na mshirika wake. Na ninashuhudia ya kwamba Bwana wetu na Mtume wetu Muhammad, S.A.W, ni Mja na Mjumbe wake. Ewe Mola wetu, Mswalie, na umrehemu na umbariki yeye na Jamaa zake na Maswahaba wake wote mpaka siku ya Mwisho.

Ndugu zangu Waislamu:

Hakika kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu kuna Athari kubwa ambapo Mja huchuma Matunda yake Duniani na Akhera. Miongoni mwake ni: Kwamba atakaeingia katika kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu basi Mwenyezi Mungu Mtukufu atamponda na kila aina ya Shari na atamwondoshea kila lenye madhara.

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{الَّذِينَ قَالَ لَهُمُ النَّاسُ إِنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعُوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إِيمَانًا وَقَالُوا حَسْبُنَا اللَّهُ وَنِعْمَ الْوَكِيلُ}

Walio ambiwa na watu: Kuna watu wamekukusanyikieni, waogopeni! Hayo yakawazidishia Imani, wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosha, naye ni mbora wa kutegemewa.

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَمَنْ يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّهِ فَهُوَ حَسْبُهُ إِنَّ اللَّهَ بَالِغُ أَمْرِهِ قَدْ جَعَلَ اللَّهُ لِكُلِّ شَيْءٍ قَدْرًا}

Na anaye mtegemea Mwenyezi Mungu Yeye humtosha. Hakika Mwenyezi Mungu anatimiza amri yake. Mwenyezi Mungu kajaalia kila kitu na kipimo chake.

 Kwa maana ya: mwenyekumtosha, Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{أَلَيْسَ اللَّهُ بِكَافٍ عَبْدَهُ}

Je! Mwenyezi Mungu si wa kumtosheleza mja wake?

Na yoyote anayemtegemea Mwenyezi Mungu Mtukufu na akamwamini vilivyo na inavyotosha, basi hakuna adui yoyote anaeweza kumdhuru yeye, na anachokitaka hakataliwi na anachokitamani hakitampita. Na tunaposimama katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Mtume wetu Musa A.S:

{وَلِتُصْنَعَ عَلَى عَيْنِي}

na ili ulelewe machoni mwangu.

 Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَاصْطَنَعْتُكَ لِنَفْسِي}

Na nimekuteuwa kwa ajili ya nafsi yangu.

 Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu akimwambia Mtume wake S.A.W:

 {وَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعْيُنِنَا}

Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu.

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَبَشِّرِ الَّذِينَ آمَنُوا أَنَّ لَهُمْ قَدَمَ صِدْقٍ عِندَ رَبِّهِمْ}

na wabashirie wale walio amini ya kuwa watakuwa na cheo cha juu kwa Mola wao Mlezi.

Tunaitambua hadhi ya Mola kuwa na Mja, na fadhila zake na athari zake Njema.

Hapana Shaka yoyote kwamba kuingia Kweli katika nafasi ya kuwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu na kuwa chini yake ni katika Milango Muhimu mno ya Utulivu wa Mja, na kutulizana kwa moyo na kuwa na afya njema ya nafsi yake, na ni njia ya kujiepusha na kila upande wa ukosefu wa utulivu wa nafsi, Wasiwasi, mgongano wa mawazo, na msongo wa mawazo. Kwani vipi Mja anaweza kuwa na wasiwasi kama atafuata njia sahihi na akatambua ya kwamba jambo lolote liko katika mikono ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na anapoamua kitu husema kuwa na kikawa?.

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{قُلِ اللَّهُمَّ مَالِكَ الْمُلْكِ تُؤْتِي الْمُلْكَ مَنْ تَشَاءُ وَتَنْزِعُ الْمُلْكَ مِمَّنْ تَشَاءُ وَتُعِزُّ مَنْ تَشَاءُ وَتُذِلُّ مَنْ تَشَاءُ بِيَدِكَ الْخَيْرُ إِنَّكَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ}

Sema: Ewe Mwenyezi Mungu uliye miliki ufalme wote! Wewe humpa ufalme umtakaye, na humwondolea ufalme umtakaye, na humtukuza umtakaye, na humuangusha umtakaye. Kheri yote iko mikononi mwako. Hakika Wewe ni Muweza wa kila kitu.

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{ما يَفْتَحِ اللَّهُ لِلنَّاسِ مِن رَّحْمَةٍ فَلَا مُمْسِكَ لَهَا  وَمَا يُمْسِكْ فَلَا مُرْسِلَ لَهُ مِن بَعْدِهِ  وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ}

Rehema ambayo Mwenyezi Mungu anawafungulia watu hapana wa kuizuia. Na anayo izuia hapana wa kuipeleka isipo kuwa Yeye. Naye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.

Hakika Waja wa Mwenyezi Mungu Mtukufu kuhisi kuwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu na kuusogeza Utukufu wake katika nyoyo zao, huwafsnikishia wao na Jamii yao viwango vya juu vya daraja la amani na usalama wa kijamii kwani Waja wanapojua kwa uyakinifu Kwamba wao kamwe hawatoweki machoni mwa Mwenyezi Mungu Mtukufu basi maadili yao hunyooka na Tabia zao zikawa nzuri, wakawa wanafuata maamrisho yake Mwenyezi Mungu Mtukufu na wanajiepusha na Makatazo yake Mwenyezi Mungu Mtukufu na wanasimama katika Mipaka yake na wanafanya kazi ili watengeneze Dunia kwa Dini yao. Na kila mmoja wao akawa anaishi kwa amani katika nafsi yake na katika Familia yake na ndugu zake anaowalea yeye, na Majirani zake, wenzake marafiki zake na Jamii yake na Watu wote. Na hiyo ndiyo Risala ya Uislamu aliyokuja nayo Mtume Muhammad, ambaye ni Rehma kwa Viumbe vyote.

Ewe Mola wetu Mtukufu, tunakuomba utuingize katika Wale unaowanusuru na kuwasaidia, na tukauomba utuongezee Fadhila zako, na utupanulie neema zako kwetu, na uturuzuku Nia njema katika mambo yetu yote na Uilinde Nchi yetu na nchi zote Duniani.

 

_____________________________

للإطلاع علي قسم خطبة الجمعة

 

تابعنا علي الفيس بوك

 

الخطبة المسموعة علي اليوتيوب

 

للإطلاع علي قسم خطبة الجمعة باللغات

 

للإطلاع ومتابعة قسم خطبة الأسبوع

 

للمزيد عن أخبار الأوقاف

 

للمزيد عن أسئلة امتحانات وزارة الأوقاف

 

للمزيد عن مسابقات الأوقاف

عن كتب: د.أحمد رمضان

الدكتور أحمد رمضان حاصل علي الماجستير من جامعة الأزهر بتقدير ممتاز سنة 2005م ، وحاصل علي الدكتوراه بتقدير مع مرتبة الشرف الأولي من جامعة الأزهر الشريف سنة 2017م. مؤسس جريدة صوت الدعاة ورئيس التحرير وكاتب الأخبار والمقالات المهمة بالجريدة، ويعمل بالجريدة منذ 2013 إلي اليوم. حاصل علي دورة التميز الصحفي، وقام بتدريب عدد من الصحفيين بالجريدة. للتواصل مع رئيس التحرير على الإيميل التالي: [email protected] رئيس التحريـر: د. أحمد رمضان (Editor-in-Chief: Dr. Ahmed Ramadan) للمزيد عن الدكتور أحمد رمضان رئيس التحرير أضغط في القائمة علي رئيس التحرير

شاهد أيضاً

خطبة الجمعة النبي معلمًا ومربيًا مترجمة إلى تسع عشرة لغة أجنبية و word pdf

خطبة الجمعة النبي معلمًا ومربيًا مترجمة إلى تسع عشرة لغة أجنبية و word pdf

في إطار حملة نبي الرحمة التي أطلقتها وزارة الأوقاف مطلع ربيع الأنور تزامنًا مع احتفالها …

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : "فضل الشهادة ومنزلة الشهيد وفلسفة الحرب في الإسلام"، بتاريخ 2 ربيع الأول 1443هـ - الموافق 8 أكتوبر 2021م

خطبة الجمعة فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word “فضل الشهادة ومنزلة الشهيد وفلسفة الحرب في الإسلام”

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : “فضل الشهادة …

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : "إعمال العقل في فهم النص .. الإمام أبو حنيفة ومدرسته الفقهية أنموذجًا"  ، بتاريخ 24 صفر 1443هـ - الموافق 1 أكتوبر 2021م

خطبة الجمعة فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : “إعمال العقل في فهم النص ..

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : “إعمال العقل …

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : حق الوطن والمشاركة في بنائه ، بتاريخ 10 صفر 1443هـ - الموافق 17 سبتمبر 2021م

خطبة الجمعة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : حق الوطن والمشاركة في بنائه

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : حق الوطن …

اترك تعليقاً

لن يتم نشر عنوان بريدك الإلكتروني. الحقول الإلزامية مشار إليها بـ *

هذا الموقع يستخدم Akismet للحدّ من التعليقات المزعجة والغير مرغوبة. تعرّف على كيفية معالجة بيانات تعليقك.

Translate »