web analytics
أخبار عاجلة
Sunna Tukufu ya Mtume S.A.W, na Nafasi yake katika Sheria
Sunna Tukufu ya Mtume S.A.W, na Nafasi yake katika Sheria

Sunna Tukufu ya Mtume S.A.W, na Nafasi yake katika Sheria

Sunna Tukufu ya Mtume S.A.W, na Nafasi yake katika Sheria

خطبة الجمعة القادمة لوزراة الأوقاف المصرية والخطبة المسموعة باللغة السواحلية : السنة النبوية المشرفة ومكانتها في التشريع ، بتاريخ 21 فبراير 2020 م ، 27 جمادي الثانية 1441 هـ .

 

 

video

 

Sifa zote njema ni zake Mwenyezi Mungu Mtukufu Mola Mlezi wa viumbe vyote, anaesema katika Kitabu chake Kitukufu:

{وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانْتَهُوا وَاتَّقُوا اللَّهَ إِنَّ اللَّهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ}

Na anacho kupeni Mtume chukueni, na anacho kukatazeni jiepusheni nacho. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.

Na ninashuhudia ya kwamba hakuna mungu mwingine yoyote anaestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, yeye pekee asiye na mshirika wake. Na ninashuhudia ya kwamba Bwana Wetu na Mtume wetu Muhammad Ni Mja na Mjumbe wake. Ewe Mola Wetu Mlezi tunakuomba umswalie umrehemu na umbariki yeye na Jamaa zake na Maswahaba wake na kila mwenyekuwafuata, Mpaka Siku ya Malipo.

Na baada ya Utangulizi huu:

Mwenyezi Mungu Mtukufu ameituma Mitume yake na Manabii A.S, kwa lengo la kuwaongoza Watu, na kuwashika mikono yao ili wawatoe kwenye giza na kuwapeleka katika nuru, na kuwatoa katika njia ya kuangamia na kuwapeleka njia ya Wokovu na Kufuzu, ambapo anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{لَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلَنَا بِالْبَيِّنَاتِ وَأَنْزَلْنَا مَعَهُمُ الْكِتَابَ وَالْمِيزَانَ لِيَقُومَ النَّاسُ بِالْقِسْطِ}

Kwa hakika tuliwatuma Mitume wetu kwa dalili waziwazi, na tukateremsha Kitabu pamoja nao na Mizani, ili watu wasimamie uadilifu.

Kisha Mwenyezi Mungu Mtukufu akazikamilisha risala zote kupitia Mtume wetu Muhammad, S.A.W, akaja Mtume S.A.W, kama asemavyo Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{شَاهِدًا وَمُبَشِّرًا وَنَذِيرًا * وَدَاعِيًا إِلَى اللَّهِ بِإِذْنِهِ وَسِرَاجًا مُنِيرًا}

Ewe Nabii! Hakika Sisi tumekutuma uwe shahidi na mbashiri na mwonyaji, Na mwitaji kumwendea Mwenyezi Mungu kwa idhini yake, na taa yenye kutoa nuru.

Kwa Ujumbe wa mwisho unaokamilisha kila kitu, unaofaa zama zozote na sehemu yoyote. Na akamteremshia Qurani tukufu kitabu kilichoandaliwa vyema na muujiza. Hakufikiri na batili kwa upande wowote, kisha Mtume S.A.W, akateremshiwa Wahyi wa Sunna tukufu inayokitafsiri Kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kukisherehesha ipasavyo, mbapo anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وما ينطِقُ عَنِ الهَوَى * إنْ هُوَ إلاّ وَحْيٌ يُوحَى}

Wala hatamki kwa matamanio. Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa.

Na anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَأَنزَلْنَا إِلَيْكَ الذِّكْرَ لِتُبَيِّنَ لِلنَّاسِ مَا نُزِّلَ إِلَيْهِمْ وَلَعَلَّهُمْ يَتَفَكَّرُونَ}

Nasi tumekuteremshia wewe Ukumbusho ili uwabainishie watu yaliyo teremshwa kwao, wapate kufikiri.

Na anasema Mtume wetu S.A.W: Tambueni kwamba Mimi nimepewa Qurani na Mfano wake pamoja na hiyo Qurani.

Na mwenye kukizingatia kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu anakuta kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu amekusanya baina ya maamrisho yake na maamrisho ya Mtume wake S.A.W, katika zaidi ya sehemu moja: anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ}

Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele.

Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ameambatanisha baina ya kumridhia yeye na kumridhia Mtume S.A.W, katika kauli yake yeye aliyetukuka:

{وَاللَّهُ وَرَسُولُهُ أَحَقُّ أَنْ يُرْضُوهُ إِنْ كَانُوا مُؤْمِنِينَ}.

hali ya kuwa wanao stahiki zaidi kuridhishwa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake, lau kama wao ni Waumini.

Vilevile Mwenyezi Mungu Mtukufu ameambatanisha kumtii yeye na kumtii Mtume wake S.A.W. anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{مَنْ يُطِعِ الرَّسُولَ فَقَدْ أَطَاعَ اللَّهَ}

Mwenye kumtii Mtume basi ndio amemtii Mwenyezi Mungu.

Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ameujaalia Utiifu ukawa ni sababu ya Rehma. Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَأَطِيعُوا اللَّهَ وَالرَّسُولَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ}

Na mt’iini Mwenyezi Mungu na Mtume ili mpate kurehemewa.

Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ}

…na mtiini Mtume ili mpate kurehemewa.

Na utiifu huu unapatikana kwa kuifuata Sunna ya Mtume S.A.W. Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{قُلْ إِنْ كُنْتُمْ تُحِبُّونَ اللَّهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَاللَّهُ غَفُورٌ رَحِيمٌ}.

Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu.

Wanachuoni wa Uma wamekubaliana Wote juu ya Hadithi tukufu za Mtume Wetu S.A.W, kuwa ni hoja. Na kwamba Hadithi ni chanzo kikuu cha pili cha Sheria baada ya Qurani tukufu. Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَأَنزَلَ اللَّهُ عَلَيْكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَعَلَّمَكَ مَا لَمْ تَكُنْ تَعْلَمُ وَكَانَ فَضْلُ اللَّهِ عَلَيْكَ عَظِيمًا}

Na Mwenyezi Mungu amekuteremshia Kitabu na hikima na amekufundisha uliyo kuwa huyajui. Na fadhila za Mwenyezi Mungu zilizo juu yako ni kubwa. Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَاذْكُرْنَ مَا يُتْلَى فِي بُيُوتِكُنَّ مِنْ آيَاتِ اللَّهِ وَالْحِكْمَةِ إِنَّ اللَّهَ كَانَ لَطِيفًا خَبِيرًا}

Na kumbukeni yasomwayo majumbani mwenu katika Aya za Mwenyezi Mungu na hekima. Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo ya siri, na Mwenye khabari.

Na Sunna tukufu inakusanya: Maneno yake Mtume S.A.W, Vitendo vyake, na kuyakubali kwake yanayofanyika mbele yake. Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ لِّمَن كَانَ يَرْجُو اللَّهَ وَالْيَوْمَ الْآخِرَ وَذَكَرَ اللَّهَ كَثِيرًا}

Hakika nyinyi mnayo ruwaza njema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa anaye mtaraji Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na akamkumbuka Mwenyezi Mungu sana.

Na hii ni katika hali zake zote S.A.W. kutoka kwa Abdullahi bin Amri R.A, amesema: Mimi nilikuwa nikiandika kila kitu ninachokisikia kutoka kwa Mtume S.A.W, na kutaka Kukihifadhi kichwani, basi Makureshi wakanizuia nisifanye hivyo, na wakasema: unaandika kila kitu unachokisikia kutoka kwa Mtume S.A.W, na Mtume S.A.W, anazungumza akiwa katika hali ya kuridhika na katika hali ya ghadhabu? Nikajizuia kufanya hivyo. Kisha nikayasema Maneno haya kwa Mtume S.A.W, akaashiria kwa mkono wake kwenye mdomo Wake, na akasema: Andika, na ninaapa kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake hakitoki kwa kwake isipokuwa Ukweli.

Kwa hiyo Qurani tukufu Ndio Chimbuko kuu la kwanza la Sheria, na Sunna ya Mtume wetu S.A.W, iliyosalia ni Chimbuko kuu la pili la Sheria, ambapo Sunna inaisherehesha, inaofafanua na kutafsiri yaliyomo ndani ya Qurani tukufu, kwani Mtume S.A.W ndiye anayejua zaidi kilichokusudiwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Kitabu chake, na jinsi Mtume anavyopitisha hukumu, na hukumu zake kuhusu Maamuzi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na hekima zake. Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

يَتَكَلَّمُ فِي الرِّضَا وَالْغَضَبِ ؟

{وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلَا مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَمْرًا أَن يَكُونَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ مِنْ أَمْرِهِمْ}

Haiwi kwa Muumini mwanamume wala Muumini mwanamke kuwa na khiari katika jambo, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapo kata shauri katika jambo lao.

Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤْمِنُونَ حَتَّى يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيْنَهُمْ ثُمَّ لَا يَجِدُوا فِي أَنفُسِهِمْ حَرَجًا مِّمَّا قَضَيْتَ وَيُسَلِّمُوا تَسْلِيمًا}

La! Naapa kwa Mola wako Mlezi! Hawataamini mpaka wakufanye wewe ndiye muamuzi katika yale wanayo khitalifiana, kisha wasione uzito katika nyoyo zao juu ya hukumu utayo toa, na wanyenyekee kabisa.

Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَإِذَا جَاءَهُمْ أَمْرٌ مِّنَ الْأَمْنِ أَوِ الْخَوْفِ أَذَاعُوا بِهِ وَلَوْ رَدُّوهُ إِلَى الرَّسُولِ وَإِلَى أُولِي الْأَمْرِ مِنْهُمْ لَعَلِمَهُ الَّذِينَ يَسْتَنبِطُونَهُ مِنْهُمْ}

Na linapo wafikia jambo lolote lilio khusu amani au la kitisho wao hulitangaza. Na lau kuwa wangeli lipeleka kwa Mtume na kwa wenye mamlaka kati yao, wale wanao chunguza wangeli lijua.

Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ametutahadharisha kuhusu mwenye kwenda kinyume na Amri ya Mtume S.A.W. anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{فَلْيَحْذَرِ الَّذِينَ يُخَالِفُونَ عَنْ أَمْرِهِ أَن تُصِيبَهُمْ فِتْنَةٌ أَوْ يُصِيبَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ}.

Basi nawatahadhari wanao khalifu amri yake, usije ukawapata msiba au ikawapata adhabu chungu..

Na hakika Sunna ya Mtume wetu S.A.W, ameyafafanua mengi yaliyomo ndani ya Qurani kwa kufungika. Kwa mfano imekuja Amri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ikituamrisha tuswali na tutoe Zaka ikiwa imefungua, akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَأَقِيمُوا الصَّلاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ}

Na shikeni Sala, na toeni Zaka.

Kwa hiyo, tunawezaje kuzisimamisha Nguzo za Uislamu ambazo ni Sala, Zaka, na Hija, bila ya Sunna ya Mtume S.A.W, kuweka wazi? Ambapo Mtume S.A.W, ameyabainisha hayo, akasema: Salini kama mnavyoniona Mimi ninavyosali. Akaweka wazi jinsi ya kuisali Sala kwa Vitendo vyake yeye mwenyewe. Na anasema: Utakaposimama kwa ajili ya kusali basi useme Allahu Akbar, kisha utasoma kiasi kidogo cha Qurani tukufu ulichonacho, kisha utarukuu mpaka utulizane ukiwa umerukuu, kisha utasimama na kunyooka, Kisha utasujudu mpaka utulizane ukiwa umesujudu, kisha nyakuka mpaka utulizane ukiwa umeketi, na ufanye hivyo katika Sala yako yote. Na katika Zaka, Sunna ya Mtume S.A.W, imeyabainisha mengi kuhusu vitengo vyake na akafafanua viwango vyake, na vilevile Kuhusu Hija, anasema Mtume wetu S.A.W: Jifunzeni kutoka kwangu ibada zenu za Hija.

Na alipokuja Mtu mmoja kwa Imraani bin Huswaini R.A, na akamwambia: Hizi Hadithi mnazozihadithia na mkaiacha Qurani, ni Hadithi gani hizi?  Akamwambia: Unaonaje kama wewe na wenzako mngeileta Qurani tukufu mngelijuaje kuwa Sala ya Adhuhuri iko hivi na vile? Na Sala ya Alasiri iko hivi na vile, na wakati wake ni huu au ule? Na sala ya Magharibi iko hivi na vile? Na Kisimamo cha Arafa na kurusha vijiwe ni hivi na vile…?

Sunna ya Mtume S.A.W, pia imepambanua aya zinazohitaji ufafanuzi katika Qurani tukufu na pia Sunna inaweza kukiwekea mipaka maalumu kisichokuwa na mipaka, na kwa ajili hiyo, imefungamanisha Wasia na theluthi moja ya Mali, na Mrithi kutokuwa na Wasia.  Kutoka kwa Saad bin Waqaas R.A, amesema: Mtume S.A.W, alikuwa ananitembelea mimi nilipokuwa mgonjwa nilipokuwa Maka. Nikamwambia kwamba mimi nina Mali je ninaweza kuusia mali yangu yote? Akasema Mtume: Hapana. Nikasema: Nusu ya mali yangu je? Akasema Mtume: Hapana. Nikasema: Je theluthi moja? Akasema: Theluthi moja tu. Na theluthi moja ni nyingi, unapowaacha warithi wako wanajitosheleza ni bora zaidi kuliko kuwaacha wakiwa masikini wanawaomba omba Watu wengine…

Sunna imebainisha vilivyo ya kwamba Wasia hauwi kwa Warithi, ambapo Mtume S.A.W, anasema: Mrithi hana Wasia. Sunna imebainisha pia uharamu wa kuwakusanya kindoa mwanamke na shangazi yake au mwanamke na mama yake mdogo. Anasema Mtume wetu S.A.W: Mwanamke haolewi pamoja na Shangazi yake au Mama yake Mdogo.

Ninaisema kauli yangu hii na ninamwomba Mwenyezi Mungu Mtukufu msamaha kwa ajili yangu na yenu.

*     *      *

Sifa zote njema ni zake Mwenyezi Mungu Mtukufu Mola Mlezi wa viumbe vyote. Na ninashuhudia ya kwamba hakuna mungu mwingine yoyote anaestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, yeye pekee asiye na mshirika wake. Na ninashuhudia ya kwamba Bwana Wetu na Mtume wetu Muhammad Ni Mja na Mjumbe wake. Ewe Mola Wetu Mlezi tunakuomba umswalie umrehemu na umbariki yeye na Jamaa zake na Maswahaba wake na kila mwenyekuwafuata, Mpaka Siku ya Malipo.

Ndugu zangu Waislamu:

Na sisi tukiwa tunaisisitizia nafasi muhimu ya Sunna na kuwa kwake Hoja na vilevile nafasi yake katika Sheria, hakika sisi – wakati huo huo – tunatofautisha kwa Uwazi baina ya zile Sunna za Ibada mbali mbali, na yaliyomo katika matendo ya mila na desturi ambazo hubadilika kwa kubadilika zama na sehemu, na mila na desturi za Watu ni kama zile zinazohusiana na mavazi, njia za usafiri na mengine mengi ambayo yanarejea katika mazoea ya Watu, kwa hivyo kila zama zina mila na desturi zake ambazo ni tofauti na zilizokuwa kabla yake. Na haiingii akilini kusema kwamba Watu walazimishwe mila na desturi fulani safarini au vazi fulani au chakula fulani kwa hoja ya kumfuata Mtume S.A.W. kwani marejeo ya mila na desturi ni katika vile walivyozoea Watu na ambavyo vinaendana na wakati pamoja na mazingira yao, na havikiuki yaliyo thabiti katika Sheria ya Uislamu.

Na Imamu Shafi alipohesabia kuwa kofia au kitambaa cha kufunika kichwa ni katika vitu vya lazima kwa mwenye Maadili Mema, hiyo ilitokana na kuchunga hali ya mazingira yake na zama zake, na leo hakuna utata katika hilo; kwani mila na desturi pamoja na mwonjo vyote havilipingi jambo hili.

Tunathibitisha ya kwamba maadui wakubwa zaidi wa Sunna ni wa aina mbili: aina ya kwanza: Ni wale wanaojitajirisha kupitia Dini na ambao wanaipotosha na wao hutumia sehemu za Maandiko zilizocheza kwa ajili ya malengo yao maalumu, wakamwaga damu na kubomoa kwa jina la Dini na wanajihesabia kwamba wao wanatengeneza vilivyo, ila ukweli ni kwamba Dini haina uhusiano wowote na Watu hawa, na hawa ndio wale aliotuonya Mtume S.A.W, katika kauli yake: Wameangamia wenye kujikweza katika Dini. Akakariri maneno haya mara tatu. Na kutoka kwa Omar bin Khatwaab, R.A, kwamba Mtume S.A.W, amesema: Hakika jambo la kutisha zaidi ninaloliogopa juu ya Uma Wangu ni kila Mnafiki mwenye ulimi wenye maneno mazuri na ya kuvutia.

Na aina ya pili: ni wale ambao hawajachukua wao wenyewe Nuru ya Elimu na nyenzo zake, na Mtume S.A.W, amebainisha hatari ya Watu hawa akasema: Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu haondoshi elimu kwa kuipokonya kwa Wanachuoni katika waja wake, lakini huiondosha elimu kwa kuwaondosha Wanachuoni, mpaka asibakishwe hata mwana huoni mmoja, na hapo ndipo Watu wanapowafanya wajinga kuwa viongozi wao, wakaulizwa maswali na wakafutu Masuala mbalimbali bila ya kuwa na elimu, wakapotoka na kupotosha.

Kwa hiyo, Sunna ya Mtume S.A.W, haina hatia yoyote ya misimamo mikali inayojiengua na Usamehevu wa Uislamu na Mfumo wake. Na misimamo mikali inakanushwa kikamilifu na Sheria ambapo Mtume S.A.W, anasema: Mtu aliyeketi katika kiti chake anakaribia kuzungumza kwa Hadithi yangu mimi, anasema: baina yangu mimi na nyinyi ni Kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu, tutakachokikuta ndani yake kilicho halali nasi tutakihalalisha, na kitakachokuwa ndani yake ni Haramu na Sisi tunakiharamisha. Hakika mambo yalivyo ni kwamba alichokiharamisha Mtume S.A.W, ni sawa na alichokiharamisha Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Hakika kujikweza kidini na kupindukia ni Ukali ulio mbali na Usamehevu wa Uislamu na Mfumo wake, na ni kuidhulumu Sunna ya Mtume S.A.W kwa kiasi kikubwa mno, Sunna ambayo inapangika na kuratibika kwa kila mpangilio na uratibu na Makusudio Makuu ya Qurani tukufu, na kwa kuyaelewa Makusudio yake tutakuwa tumesimama katika Makusudio Makuu ya Dini yetu tukufu, na bila ya shaka huu ndio Uadilifu Kamili, Rehma Kamili, Usamehevu Kamili, Uwepesishaji Kamili, na Utu Kamili. Na Wanachuoni hapo zamani na hivi sasa, wanakubaliana kwamba kila kitakachoyafikia Malengo haya Makubwa ni katika Undani wa Uislamu, na mtu  hagongani nayo isipokuwa atakuwa  anagongana na Uislamu na Malengo na Makusudio yake.

Na hapo ndipo unapokuja mchango wa Wanachuoni wabobezi katika kunyoosha makosa ya Watu wa upotofu na ukengeukaji ambapo anasema Mtume wetu S.A.W: Elimu hii hubebwa na waadilifu wa kila wanaowafuatia wakawakanusha wapotovu wenye kudai Kuwa wana elimu, na kuwakanusha wajinga wenye kutafsiri watakavyo, na upotoshaji wa wenye misimamo mikali.

Hakika sisi tuna haja ya kuifahamu Sunna ya Mtume wetu S.A.W, kupitia Makusudio yake Makuu na Malengo yake, na tusiwe wang’ang’anizi tusiokubali kubadilika tukang’ang’ania uwazi wa Maandiko bila ya kufahamu kwa kina peo zake na Makusudio yake, na hili kinapatikana kwa kuyasoma Makusudio yake ya zama hizi ya Sunna ya Mtume S.A.W, inayoendana na uhalisia wa zama hizi na mapya yanayojitokeza na kuisogeza Sunna kwa Watu. Na huu ndio ubunifu unaolinganiwa na Sunna iliyo twaharika, ambapo anasema Mtume Wetu S.A.W: Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu anauletea Uma huu Katika kila miaka mia moja Mtu atakayeleta ubunifu wa Dini yao.

Ewe Mola Wetu Mlezi tunakuomba utuwafikishe tukijue kitabu chako Kitukufu na Sunna ya Mtume wako S.A.W, na tunakuomba utufundishe yanayotunufaisha, na utunufaishe kwa elimu uliyotufundisha, na Uzilinde Nchi zetu na Nchi zote Duniani.

Amin.

 

_____________________________

للإطلاع علي قسم خطبة الجمعة

 

تابعنا علي الفيس بوك

 

الخطبة المسموعة علي اليوتيوب

 

للإطلاع علي قسم خطبة الجمعة باللغات

 

للإطلاع ومتابعة قسم خطبة الأسبوع

 

للمزيد عن أخبار الأوقاف

 

للمزيد عن أسئلة امتحانات وزارة الأوقاف

 

للمزيد عن مسابقات الأوقاف

عن كتب: د.أحمد رمضان

الدكتور أحمد رمضان حاصل علي الماجستير من جامعة الأزهر بتقدير ممتاز سنة 2005م ، وحاصل علي الدكتوراه بتقدير مع مرتبة الشرف الأولي من جامعة الأزهر الشريف سنة 2017م. مؤسس جريدة صوت الدعاة ورئيس التحرير وكاتب الأخبار والمقالات المهمة بالجريدة، ويعمل بالجريدة منذ 2013 إلي اليوم. حاصل علي دورة التميز الصحفي، وقام بتدريب عدد من الصحفيين بالجريدة. للتواصل مع رئيس التحرير على الإيميل التالي: [email protected] رئيس التحريـر: د. أحمد رمضان (Editor-in-Chief: Dr. Ahmed Ramadan) للمزيد عن الدكتور أحمد رمضان رئيس التحرير أضغط في القائمة علي رئيس التحرير

شاهد أيضاً

خطبة الجمعة النبي معلمًا ومربيًا مترجمة إلى تسع عشرة لغة أجنبية و word pdf

خطبة الجمعة النبي معلمًا ومربيًا مترجمة إلى تسع عشرة لغة أجنبية و word pdf

في إطار حملة نبي الرحمة التي أطلقتها وزارة الأوقاف مطلع ربيع الأنور تزامنًا مع احتفالها …

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : "فضل الشهادة ومنزلة الشهيد وفلسفة الحرب في الإسلام"، بتاريخ 2 ربيع الأول 1443هـ - الموافق 8 أكتوبر 2021م

خطبة الجمعة فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word “فضل الشهادة ومنزلة الشهيد وفلسفة الحرب في الإسلام”

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : “فضل الشهادة …

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : "إعمال العقل في فهم النص .. الإمام أبو حنيفة ومدرسته الفقهية أنموذجًا"  ، بتاريخ 24 صفر 1443هـ - الموافق 1 أكتوبر 2021م

خطبة الجمعة فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : “إعمال العقل في فهم النص ..

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : “إعمال العقل …

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : حق الوطن والمشاركة في بنائه ، بتاريخ 10 صفر 1443هـ - الموافق 17 سبتمبر 2021م

خطبة الجمعة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : حق الوطن والمشاركة في بنائه

خطبة الجمعة القادمة لوزارة الأوقاف فيديو مسموعة وباللغات و pdf و word : حق الوطن …

اترك تعليقاً

لن يتم نشر عنوان بريدك الإلكتروني. الحقول الإلزامية مشار إليها بـ *

هذا الموقع يستخدم Akismet للحدّ من التعليقات المزعجة والغير مرغوبة. تعرّف على كيفية معالجة بيانات تعليقك.

Translate »